Hakuna vibali vya kuingiza sukari kwa sasa



Serikali imesema kuwa itasimamia sheria na taratibu ilizojiwekea kwenye usimamizi wa mazao mbalimbali ikiwemo miwa, hivyo haitatoa kibali kwa wafanyabiashara wa sukari badala yake kibali kitatolewa kwa wazalishaji wa ndani kama kutakuwa na uhitaji.

Imebainisha kuwa kwa sasa nchini kuna ziada ya Tani Zaidi ya 70,000 za sukari hivyo serikali haiwezi kutoa kibali chochote cha uagizaji wa sukari nje ya nchi wakati uzalishaji unaendelea nchini.

Waziri wa Kilimo, Prof. Adolf Mkenda amesema serikali kuendelea kutoa kibali kuagiza sukari nje ya nchi sio sahihi kwani inahatarisha uzalishaji wa sukari nchini jambo linalowakosesha ajira watanzania wengi huku likiwakosesha soko la miwa kwa wakulima ambao miwa yao huchomwa kutokana na uwezo mdogo wa viwanda vya ndani.

Comments