Trump kurudi kama mgombea urais mwaka 2024

   

 


Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump, alitoa ishara kwamba anaweza kugombea tena kwenye uchaguzi wa urais utakaofanyika mwaka 2024.


Donald Trump, ambaye alimkabidhi madaraka ya urais mpinzani wake wa Kidemokrasia Joe Biden mnamo Januari 20, alitoa hotuba yake ya kwanza kwa umati katika Mkutano wa Hatua ya Kisiasa ya 2021 huko Florida.


Akihutubia umati wa watu katika ukumbi uliofurika, Trump alikosoa utawala wa Biden, na kutoa maoni yake juu ya mustakabali wa yeye mwenyewe na Chama cha Republican.


Kwa kutumia maneno yake ya "Kwani hamjanitamani?", Trump alisema kuwa harakati za kisiasa walizoanzisha miaka 4 iliyopita hazijaisha, na wameanza msafara wao.


Trump ambaye anakanusha wazi madai ya chama kipya, pia alisema,


"Sitaanzisha chama kipya, taarifa hizo ni za uwongo. Chama cha Republican ni chama chetu. Harakati zetu za Wamarekani wenye kujivunia, wachapakazi na wazalendo zimeanza, na mwishowe tutashinda."


Akirudia madai ya udanganyifu katika uchaguzi, Trump alisema kwamba majukwaa ya mitandao ya kijamii kama vile Twitter na Facebook  yanalenga kufunga akaunti za wanachama nchini, na kampuni hizo zinapaswa kuchunguzwa.

Comments