DC Godwin Gondwe afanya ziara ya kushtukiza katika soko jipya la Magomeni


Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Godwin Gondwe leo amefanya ziara ya kushtukiza katika soko jipya la Magomeni ambapo amezunguka kwenye soko hilo na kusikiliza kero za Wafanyabiashara walioingia ndani ya soko na kisha kuahidi kuzifanyia kazi.

Kero kubwa aliyokutana nayo DC Gondwe ni kutoka kwa Wafanyabiashara wanaouza bidhaa zao nje ya soko ambapo ameahidi kutolea tamko suala hilo.

 

Comments